Sunday, January 14, 2024

NAPENDA KUWATAKIENI KHERI SANA YA MWAKA MPYA 2024

Kwanza kabisa napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutulinda sisi wote kwa kuona Mwaka 2024. Wengi walitamani kuona lakini haikuwa bahati kwao.Binafsi mimi na familia yangu tu- wazima wa afya njema na ninaamini hata wewe usomaye hapa utakuwa mzima wa afya na wanaokuzunguka. Kwa hiyo basinachukua nafasi hii kuwatakieni wote mtakaopita hapa AMANI NA FURAHA VITAWALE MIONYONI MWENU . Tutaonana tena karibuni// mama Maisha na Mafanikio/ Kapulya

Sunday, November 19, 2023

Saturday, September 16, 2023

NYUMBA :- NIMEPENDA ZILIVYOKAA

JUMAMOSI NJEMA WANDUGU!...NI MIE KAPULYA WENU

Sunday, July 9, 2023

Sunday, May 14, 2023

Wednesday, January 18, 2023

KHERI SANA YA MWAKA MPYA 2023

!
Ndugu zanguni wapendwa napenda kuwatakieni kheri sana kwa mwaka mpya 2023. Najua nimechelewa kidogo lakini salamu hazina kuchelewa natumaini wote mu-wazima waafya njema na mwaendelea na majukumu ya kila siku. Tuzidi kumwomba Mungu kwa wote anayotubariku. NAPENDA KUWATAKIENI AMANI NA UPENDO PIA FURAHA. nI MIMI KAPULYA WENU

Tuesday, December 20, 2022

UJUMBE WA JIONI YA LEO

Binadamu hataki kuwa alivyo. Isipokuwa anafikiri angekuwa binadamu wa aina gani! NAWATAKIENI JIONI YENYE AMANI NA FURAHA!

Saturday, August 20, 2022

TUMAZE WIKI NA UJUMBE HUU!

NIMETUMIWA HUU UJUMBE NIMEONA NISIWE MCHOYO WA ELIMU:- Nyoka uliyembeba kwenye mzigo wa kuni kutoka shambani anaweza kukuumia nyumbani wakati unatua mzigo. Siyo kila unayemsaidia lazima akusaidie, wengine inabidi wakuumize ili ujifunze. Kuna watu wanajifunza vizuri baada ya kuumizwa. Kwa hiyo katika maisha tunahitaji watu wote; wazuri na wabaya. Wazuri watakupa furaha, wabaya watakupa uzoefu ndiyo maana imeandikwa mpende adui yako, ila angalia asikuue, maana ukifa hutojifunza kitu! Imeandikwa na Mwl. Denis Mpagaze.

HAYA NDIYO MATOKEO: UTAKULA ULICHOPANDA NA HII NDIYO KAZI YA MIKONO YANGU

TUNAKULA NYANYA ZETU MPAKA KUSAZA....

Monday, April 25, 2022

NAPENDA KUWATAKIENI MWANZO MWEMA WA WIKI NDUGU ZANGU!

NIMEYAPENDA HAYA MAZINGIRA KWA KWELI YAONEKANA NI SEHEMU NZURI NA YA UTULIVU.

Thursday, April 14, 2022

TANZIA:_ NIMEFIWA NA MAMA YANGU MDOGO HUKO MBEYA LEO MCHANA

Mama tulikupendda sana ila Baba wa Mbinguni kakupenda zaidi. Pumzika kwa amani mama yangu

Wednesday, January 26, 2022

Monday, November 29, 2021

NARUDI NYUMBANI:- LAKINI KWA MUDA TU!

NI RAHA ILIOJE KUWENDA NYUMBANI KULA LIKOLO LA NANYUNGU! TUTAONANA SI MUDA MREFU

Wednesday, October 6, 2021

VYAKULA VYA ASILI NI MUHIMU SANA

Tusisahau vyakula vyetu vya asili. Maana hapo utakuwa umesahau ulikotoka.

Friday, September 3, 2021

UJUMBE WA WIKI HII!

Watu watano wanaostahili muda wako:- 1. Familia 2. Rafiki(bora) wa karibu 3. Mshauri/mlezi wako 4. Wanaohitaji msaada wako 5. Wewe mwenyewe yapaswa:- Ujipende na utumie muda wako kutafakari na kujiboresha.

Saturday, August 21, 2021

Wednesday, June 9, 2021

LEO MWENZENINIMEKUMBUKA NYASA KWETU NA KITU HII LIKUNGU..NI MBOGA TAMU SANA

KATI YA VYAKULA NIVIPENDAVYO MOJAWAPO NI LIKUNGU HASA LIKIWA MADAFU